dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Saturday, July 25, 2015

Amini usiamini: Lowassa sasa rasmi Ukawa

Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa (kulia) akiwa na Mnadhimu Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Tundu Lissu wakiwa katika mazungumzo walipokutana hivi karibuni jijini Dar.

Na Neophitius Kyaruzi, GPL

BAADA ya vuta nikuvute katika vyama vya siasa vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kuhusu kukubaliwa au kutokubaliwa kwa Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Ngoyai Lowassa kujiunga na umoja huo ili kuongeza nguvu ya kisiasa, hatimaye mwanasiasa huyo maarufu nchini amekubaliwa na tayari amejiunga rasmi Ukawa akiwa mwanachama halisi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), imefahamika.

Taarifa rasmi kutoka Ukawa na kwa msemaji wa Lowassa ambaye hakutaka jina lake litajwe, imeeleza kuwa uamuzi huo ulifikiwa baada ya majadiliano ya kina katika Mkutano Mkuu wa Ukawa uliofanyika mapema wiki hii huku ajenda kubwa ikiwa ni kumpokea Lowassa ili kuimarisha kambi ya upinzani ikiwa ni pamoja na kumsimamisha kama mgombea urais wa umoja huo.

Taarifa rasmi zilizolifikia gazeti hili zimeeleza kuwa Lowassa anatarajiwa kutangazwa rasmi Jumapili hii hivyo maadalizi ya mkutano mkubwa wa aina yake yanaendelea. Chanzo chetu kutoka katika mkutano huo kilisema kwa moyo mmoja, wenyeviti wa vyama vyote vinavyounda umoja huo, yaani Freeman Mbowe (Chadema), Profesa Ibrahim Lipumba (CUF), James Mbatia (NCCRMageuzi) na Emmanuel Makaidi (NLD), wameridhia kuungana na Lowassa katika safari yao ya kuking’oa CCM madarakani huku wakiamini kuwa wakimsimamisha kuwa mgombea wa Ukawa watafanikisha azma ya vyama vya upinzani kuingia ikulu. 

“Katika kikao chetu tulijadili mikakati kadhaa ya kuchukua dola lakini kubwa zaidi lilikuwa ni jinsi ya kuungana na Lowassa ili kutimiza azma hiyo, ikizingatiwa kwamba hivi sasa anaungwa mkono na Watanzania wengi na hasa jinsi ambavyo hawakuridhishwa na mchakato wa kumuengua kuwania urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), hivyo tuna uhakika kwa mkakati huu lazima tuking’oe CCM madarakani,” alisema mjumbe mmoja wa Mkutano Mkuu (jina limehifadhiwa).

TUNDU LISSU AFUNGUKA

Akizungumzia suala hilo, Mnadhimu Mkuu wa Kambi
Rasmi ya Upinzani Bungeni, Tundu Lissu, aliliambia gazeti hili kuwa majadiliano kuhusu Lowassa yalikuwa ya lazima kwa kuwa katika muungano wa vyama kila kiongozi ana mtazamo wake hivyo, kila jambo la muhimu lazima lifanyike kwa majadiliano ili kufikia mwafaka kwani lengo ni kuhakikisha kwamba kunakuwapo na mkakati wa pamoja kuhakikisha kuwa CCM kinag’olewa madarakani ili makada wa chama hicho waelewe kuwa sasa Watanzania wanahitaji mabadiliko na si maneno matupu ya majukwaani.

LIPUMBA NAYE ANENA

Kwa upande wake, Mwenyekiti Mwenza wa Ukawa, Profesa Ibrahim Lipumba alisema kwamba Ukawa hivi sasa wamejipanga kimkakati kuhakikisha wanachukua dola na kuongeza kwamba waliokuwa wakieneza propaganda kuwa anawakwamisha wataendelea kuumbuka kwa kuwa vyama vyote vinavyounda Ukawa ni kitu kimoja.

Aliongeza kwamba, kamwe umoja huo hauwezi kusambaratika kwani ajenda kuu ni kuindoa CCM madarakani na kuongeza kwamba, mambo mengine kama mgawanyo wa ruzuku yatafuata baadaye kwani yanazungumzika katika ngazi ya uongozi.

MSIMAMO WA LOWASSA

Msemaji wa Lowassa ambaye kawa sasa ndiye gumzo la taifa ukiachana na Dk. John Magufuli aliyepitishwa na CCM kuwania kiti cha urais amelihakikishia gazeti hili kuwa Lowassa ameamua kuingia Ukawa ili kuendeleza siasa za kistaarabu kutimiza azma yake ya Safari ya Matumaini kama ambavyo amekuwa akiwaahidi Watanzania.

Alisema ameamua kuungana na Ukawa kwa kuwa anaamini kuwa lengo la vyama vyote vya siasa ni kuhakikisha vinatimiza malengo yao ya kuwahudumia wananchi, hivyo inapotokea katika chama kimojawapo, bado kuna nafasi ya kutumia vyama vingine kutimiza malengo ya kisiasa. Msemaji huyo aliongeza kwamba baada ya kuenguliwa alikuwa na kazi ngumu ya kubaini nini cha kufanya ili kutimiza azma yake ya kisiasa, ndiyo maana alikaa kimya ili kuepusha mivutano kati yake na CCM lakini hakuwa amekata tama kuhusu jinsi anavyoweza kuwakomboa Watanzania kutoka katika dimbwi la umaskini, jambo ambalo alikuwa akiwaeleza katika safari yake ya kusaka wadhamini nchi nzima.

MKAKATI WA KAMPENI

Msemaji huyo alisema kuwa akiwa katika Ukawa, Lowassa ameandaa mkakati kabambe wa uhamasishaji wananchi ili watambue kwamba azma ya kuwakomboa ipo palepale na kuongeza kuwa ana uhakika watamuunga mkono kwani anatambua kwamba wapo pamoja naye katika safari ya matumaini.

Alisema kwamba kazi iliyo mbele yake ni kuhakikisha kuwa anaisuka upya ‘Team Lowassa’ na atakuwa makini na baadhi ya watu waliomsaliti ili wasiharibu mkakati wake na kuongeza kwamba watazunguka nchi nzima kufanya kampeni za kistaarabu, zisizokashfu wanasiasa wengine ili wananchi wapime ni kiongozi gani anafaa kati ya yeye na wengine.

TATHMINI YA USHINDI

Chanzo chetu ndani ya Ukawa kilieleza kwamba, tathmini iliyofanywa hadi sasa inawapa uhakika wa kuchukua dola kwani katika maeneo mengi, Lowassa anaungwa mkono zaidi kuliko mgombea mwingine yeyote yule. Kilisema kuwa katikamaeneo mengi CCM haikubaliki kutokana na kuendesha siasa za kibabe na mizengwe, jambo ambalo limekuwa likiwakera wananchi kwani kinachotokea ni kwamba wanachaguliwa viongozi badala ya wao kuchagua viongozi wanaowataka.

Kilisema Lowassa ana nguvu zaidi katika Mikoa ya Kaskazini, Kanda ya Ziwa, Kusini, Nyanda za Juu Kusini na Zanzibar hivyo CCM kama inataka kushindana naye ijipange vyema.

ZITTO AJUMUISHWA

Katika mkakati huo wa ushindi, inaelezwa kwamba, umoja huo utamjumuisha kundini Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe ambaye chama chake nacho kitaongeza nguvu ya ushindi.

Lowassa alikuwa mgombea urais kwa tiketi ya CCM kati ya wagombea 38 ambao walichukua fomu lakini jina lake lilikatwa katika kikao cha Kamati ya Maadili na Usalama ya CCM, jambo ambalo lilizua sintofahamu miongoni mwa wanasiasa wengi waliokuwa wakimuunga mkono, hatua ambayo ilisababisha mtikisiko wa kisiasa nchini.

Chanzo: Global Publishers Ltd

No comments :

Post a Comment