dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Friday, September 23, 2016

ZACADIA YAZAWADIWA NA WAZIRI WA MAMBO YA NJE!


Kutokana na juhudi kubwa zilizochukuliwa na Jumuiya ya Wazanzibari waishio Canada - ZACADIA (Zanzibar-Canadian Diaspora Association) ya mjini Toronto, katika kutangaza na kusaidia maandalizi ya kongamano la tatu la Tanzania Diaspora lililofanyika nchini Zanzibar katika kitongoji cha Mazizini mjini Unguja, Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe Dr Augustine Mahiga, pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Zanzibar, Mhe Hon. Issa Haji Ussi Gavu, wameitunukia ZACADIA Certificate of Recognition and Appreciation for Outstanding Support of the 3rd Tanzania Diaspora Conference 2016.

Kauli mbiu ya kongamano hilo ilikuwa ni 'MTU KWAO NDIO NGAO’ ilifuatana na ujumbe mzito wa mwaka huu ambao ulikuwa ni “Mtizamo mpya wa Kuimarisha Utalii wa Tanzania na uekezaji”.

Kongamano hilo lilifanyika kwa muda wa siku mbili kati ya tarehe 24 na 25 Augosti na lilifunguliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, AlHajj Dr Ali Mohammed Shein na kufungwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli, ambae aliwakilishwa na Waziri wa Muungano Mhe Makamba, katika ukumbi wa hoteli ya Zanzibar Beach Resort.

Makachori wa Zanzibar Ni Kwetu waliohudhuria kongamano hilo wameeleza kuwa inaelekea huenda kongamano la tano likafanyika mjini Chake Chake, Pemba, wakati lile la nne huenda likafanyika mjini Dodoma au Arusha. Kongamano la kwanza na la pili yote yalifanyika mjini Dar Es Salaam.




No comments :

Post a Comment