dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Saturday, December 16, 2017

DR. SHIKA ATAKA APELEKEWE BANGKOK DOLA 1,280 KUTOKA CANADA!

SELF-PROCLAIMED BILLIONAIRE - MR. 900 ITAPENDEZA (DR. SHIKA) AKIFURAHIA MAISHA KWA UMAARUFU WA GHAFLA!

ZANZIBAR. Baada ya mwagiji fulani wa kitanzania wa kule Canada kubadilisha azma yao ya kumualika Dr. Shika na badala yake sasa kutaka kumualika Babu Seya na wanawe ambao hivi karibuni Rais Magufuli aliwaachia huru, baada ya kusota gerezani kwa miaka 13 na miezi minne wakitumikia kifungo cha maisha, Dr. Shika ameibuka tena na ombi la kutaka apelekewe Dollar 1,280 huko Bangkok, Thailand kwa jina la DARANEE SABAY na kuwa pesa hizo zitumwe kwa njia ya MoneyGram.
Katika ujumbe wake wa email uliokuenda huko Canada, Dr. Shika akiandika email yake kwa kimombo, anaelezea kuwa amerejea tena kwao kwa hao magwiji kutaka msaada.

"Ninazi-transfer pesa zangu kutoka Thailand kuja Tanzania, nishalipia insurance lakini sasa nimeganda kwenye inland revenue inayofikia Dollar 1,280 kabla pesa zangu hazijaachiwa kuja Tanzania".

Anaendelea kuandika Dr. Shika katika email yake hio kuwa, "Hapa nyumbani ninakosa msaada. Ninapewa miadi ya uwongo kwa wiki yapili sasa. Tafadhali saidia".

Copy ya email hio yapili na ile ya kwanza zikipelekwa Canada kwa jina la Lancefort Shika zote kwa sasa zipo kwenye kumbukumbu za blog la ZanzibarNiKwetu.

"Utakapozipeleka tu hizo pesa Thailand, tafadhali niletee copy ya risiti ili niifuatilie hio benki kule Thailand. Hii transfer ndio inayonichelewesha mimi kuja huko Canada", ilimalizia hio email ya Dr. Shika na huku ikiwa signed off kwa jina la Dr. Kid.

Email yenyewe kwa kizungu kama ilivyoandikwa na Dr. Shika ni hii hapa:"I am back to you pleading for help. I am transferring my funds from Thailand and I have paid for insurance, now I am stuck on inland revenue to a tune of $1,280 before my funds can be released to Tanzania. I am missing support here in Tz. I am being offered false promises for the second week now! Please HELP, send IMMEDIATELY by Money Gram the said one thousand two hundred and eighty USA Dollars to Bangkok in Thailand in the name of DARANEE SABAY and scan to me the pay slip for me to communicate with the respective bank in Thailand.

REFUNDABLE, this transfer is delaying my departure to you in Canada!


/ Dr. Kid
"

No comments :

Post a Comment